Friday 30 August 2013

Diamond amzawadia gari Ngurumo




Msanii wa bongo fleva, Nassib Abdul maarufu kama Diamond Platnumz, jana amefanya kitu cha kuishangaza jamii kwa kumzawadia gari aina ya FunCargo lenye namba za usajili T789 AYS msanii mkongwe Mzee Muhidin Gurumo wakati akizindua video yake mpya iitwayo 'Number One' katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa maoni ya wadau wameanza kutoa kauli zisizo nzuri kwa kile walichodai kuwa gari lenyewe sio jipya kutokana na nambari za usajili ni za muda kidogo au itakuwa ametoa gari lake au kamvua mtu!!

Fanya yako Diamond hata liwe la mwaka juzi mbona hakuna aliyekumbuka kufanya ivo??

BIG UP MTU MZIMA DIAMOND

No comments: