Sunday 1 November 2015

Kijana wa miaka 7 amuudumia baba yake aliyepooza mwili

Kijana mwenye umri wa miaka saba anayeishi huko kusini magharibi mwa nchi ya china anaefahamika kwa jina la Ou Yanglin amekuwa akimuuguza baba yake mzazi "Ou Tangmin" aliyepooza mwili baada ya kuanguka ghorofani alipokuwa akifanyakazi ya ujenzi.
Mtoto huyo "Ou Yanglin" amekuwa akimuudumia mzazi huyo tangu mwaka jana "2014" baada ya kukumbwa na maradhi hayo. Amesema amekuwa akipata wakati mgumu kumuuguza baba yake baada ya mama yake mzazi kuondoka na wadogo zake wenye umri wa miaka mitatu na kutorudi tena nyumbani tangu mwaka jana.
Ou Yanglin amekuwa hapati muda wa dhiada kama watoto wenzie anaosoma nao baada ya kutoka shule yeye anakosa hata muda wa kucheza, kwani amekuwa akiangaika kumuandalia chakula baba yake na kutayarisha dawa kwa aajili ya kumpa mzazi wake.

Ou Yanglin huwa anaamka mapema alfajiri saa 12 asubuh na kumuandalia chakula baba yake kabla hajaenda shule na  kisha anarudi nyumbani mida ya mchana baada ya kula chakula cha mchana cha shule anarudi nyumbani kumuandalia baba yake chakula cha mchana na kisha kurudi shuleni kwa kuendelea na masomo na baada ya masomo anaomba fedha kwa baadhi ya watu na kununua dawa kwaajili ya baba yake.

Amesema anapata taabu sana kwakuwa yeye hana fedha za kumnunulia dawa baba yake na pia mazingira ya yeye kumuuguza pia imekuwa ni mtihani mkubwa sana kwake..hivyo anaomba kama kuna wa kumsaidia kwa hilo either kumpatia dawa au fedha za kununulia dawa.

No comments: