Monday 3 August 2015

Sheria ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii yaanza kazi

Mahakama ya kisutu jijini Dar es salaam yamepokea mashtaka kutoka kwa jeshi la polisi nchini baada ya kupata "maneno ya uchochezi" yaliyotolewa na kundi lililoundwa na watu wa kwenye mtandao wa kijamii (facebook), liitwalo "TANURU LA FIKRA".... Mashtaka hayo yamefunguliwa baada ya kuwepo kwa ujumbe wa mwanakikundi huyo ambaye anafahamika kwa jina la BRUNO COLMAN KIMARYOkwa yasemekana ni mkazi wa jiji la DSM kama ilivyoelezwa hapo juu kwenye picha inayoonesha "file la kesi"..... Ndugu Bruno aliandika maneno yanayoonesha uchochezi kwa kitendo kilichofanywa na majambazi waliovamia kituo cha polisi cha STAKI SHARI na kuwaua maaskari kadhaa na kuwapora bunduki....

Hii imeonesha sasa sheria dhidi ya maneno ya matusi, masengenyo, vitisho mbalimbali imeanza kufanyiwa kazi..... kwa wale watumiaji wa hii mitandao ya kijamii ningewaomba sana muwe makini maana wengi wenu mnaitumia sivyo.

No comments: