Saturday 22 December 2012

zuma ametoa report kuhusu afya ya nelson mandela

Rais wa Afrika Kusini, bwana Jacob Zuma amewaambia viongozi wa African National Congress wakati wa kuhitimisha kikao hicho. Zuma alisema "hali ya Madiba iko serious lakini amepatiwa matibabu na ameimprove kidogo". Madiba (Mandela) mwenye miaka 94 sasa alisafirishwa kwa ndege Desemba 8 kutoka kijijini kwake huko kusini mwa nchi hiyo na kupelekwa Pretoria kwa matibabu. Hata ivo Daktari aligundua kuwa Mandela anasumbuliwa na ugonjwa wa mapafu "lung infection" na 'gallstones'. Desemba 15 alifanyiwa surgery ili kuondoa gallstones na hadi sasa bado yupo hospital anaendelea na matibabu.
Bwana Zuma amesema, kutokana na umri alionao anahitaji uangalizi mkubwa wa madaktari ili kuweza kumfanya arudi katika hali yake ya kawaida. Pia amesema Madiba ni mpiganaji shujaa na atazidi kuwa hivyo, amekutana na vikwazo vingi juu ya afya yake ila natumaini atavishinda na kuwa vyema.

No comments: