Friday 13 January 2012

KAA TAYARI KWA NGOMA MPYA KUTOKA KWA BELLE 9

 BELLE IX
Msanii wa bongofleva, Abelinago Damian alimaarufu kama Belle 9, 
leo ameviambia vyombo vya habari kuwa mashabiki na 
wapenzi wake wakae mkao wa kula kwa ngoma "nyimbo" 
yake ambayo anatarajia kuiachia kesho. Ngoma hiyo aliyoipa 
jina la AMERUDI ameifanya peke yake bila kumshirikisha 
msanii yoyote yule.
Belle 9 aliyetamba na ngoma kadhaa kipindi cha nyuma 
kama Sumu ya Penzi, Masogange, Wewe ni wangu aliyofanya 
na Blue, pia Nilipe nisepe ambayo ndio nyimbo yake 
ya mwisho kuiachia, imempa show nyingi sana kwa mwa 2011.
Anatarajia mtaipokea vizuri na kuipenda sana, 
kifupi ni muendelezo wa masogange..
kwa zaidi subiri kesho uisikie hiyo ngoma, 
nikiipata nitaitupia muweze isikiliza

No comments: