Tuesday 16 April 2013

Penny afunguka kuhusu ishu ya uwoya na Diamond

Penny akiwa na Diamond
Katika ule unaoonekana kama mwendelezo wa skendo ndani ya tasnia ya bongo movies hatimaye Jana bongomovies.com waliweza kumpata mwanadada Penny Mungilwa, mpenzi wa diamond platnumz na kufanya naye interview ya simu kuhusu stori zilizozagaa mitaani na kwenye mtandao kuhusu kipenzi cha moyo wake “Diamond Platnumz” kukutwa katika hoteli moja ya kifahari jijini Dar es salaam na mwigizaji mahiri wa bongo movies Irene Uwoya, na haya ndo yalikuwa majibu yake.

Bongomovie : Mambo penny, mzima?

Penny : Mi mzima, sijui wewe?

Bongomovie : Mi niko poa tuu, sorry nilikuwa nashida ya kukuuliza maswali mawili matatu tuu?

Penny : Kama nitaweza kuyajibu,

Bongomovie: Haina shida, kuna stori zilikuwa zimezagaa kwenye mitandao kuhusu ishu ya diamond na Irene Uwoya, sasa nilitaka niulize na nipate comment zako kuhusu ishu hizi?

Penny : Sina comment,

Bongomovie : Vipi ishu hizi ni za kweli?

Penny : Asa mi nitajuaje? Mambo afanye Diamond na Irene, mi nitajuaje?

Bongomovie: Lakini sisi tunajua kuwa wewe ndo mpenzi halali wa diamond, na stori kama hizi kwa namna moja au nyingine lazima zinakuhusu, hata kama hazipo “direct” kwako?

Penny : Naomba nikwambie kitu kimoja, wewe inabidi umtafute Irene na Diamond, mimi sina cha kukujibu, sijui kama wamefanya sijui kama hawajafanya, “I don’t have an any idea” (alisisitiza), mi sikuwepo so sijui cha kukujibu. Mi mwenyewe nimeona kama ulivyoona wewe.
Bongomovies : Ila Diamond si mtu wako wa karibu sana, si unaweza kuwa na ukweli kuhusu hili jambo?

Penny : Mi najua tuko happy, kama siku zote tunavyokuaga zamani, tuko kama tulivyokuwa juzi, jana leo na kesho, I’m happy with my baby, kama amefanya au hajafanya I don’t know, it not my business. I’m happy with my man, that’s it!!!!

Bongomovie : Vipi uhusiano wako na Irene Uwoya?

Penny: Simfahamu, na “she is not my friend” namuona kwenye magazeti tuu

Bongomovie : Okay, basi sawa,

Penny: Alright, thank you…

No comments: