Thursday 3 October 2013

Baada ya kupotea kwa muda sasa Nakaya ajitokeza na ujauzito

Nakaaya Sumari, mkali wa kibao cha "Mr. Politician" ambaye pia ni dada wa aliyewahi kuwa miss Tanzania 2005 kama sijakosea, bibie Nancy Sumari...baada ya kupotea machoni mwa watu hususani wadau wa muziki na burudani kwa ujumla kwa kutoonekana kwenye baadhi ya vyombo vya Habari kama magazeti, TV na hata kusikika kwenye redio...mwanadada huyo amejitokeza kupitia mtandao wa kijamii wa instagram akiwa amejaa tumbo (mjamzito), na kuwafanya wadau na mashabiki wake wapigwe na mshangao japo si jambo la kushangaza kuona mtu yupo katika hali hiyo, isipokuwa kuona ghafla tu Nakaaya kuonekana akiwa na ujauzito unaoashiria kujifungua baada ya muda mfupi...kitendo ambacho si raisi kwa mtu star kama yeye kuwa kimya kimya ivyo hata fununu za jamaa zetu wale wa Habari na matukio kutokujua na kuwajuza wadau!!

Hizi ni baadhi ya picha alizotupia Instagram:

No comments: