Saturday 19 October 2013

Mjue a MiniBuzz star"Kansiime Anne"

Nadhani wengi mnamfahamu huyu mwadada...ni mchekeshaji kutoka nchini Uganda kupitia video zake ambazo anazirusha youtube na kusambaa hasa kwenye simu kwa njia mbalimbali kama kwenye mitandao ya kijamii sanasana "Whatsap". Mwanadada huyo ambaye kwa jina halisi anaitwa Kansiime Anne Kubinyaba, amezaliwa na kukulia wilaya ya Kabale, nchini Uganda, ni mukiga kwa upande wa kabila, pia ni mtoto wa nne kuzaliwa toka kwenye familia ya watoto sita, ana degree ya social science....

Kwa muonekano wawezasema ni mtu wa masihala kama unavyomuona kwenye video zake akiwa kazini...kumbe ni mtu ambaye yuko tofauti kabisa na vitendo anavyofanya kwani ni mpole sana pia ni mtu wa busara na huwa si mtu wa masihala muda wote kama tunavomtizama na kumsikiliza.... 

No comments: