Sunday 26 August 2012

mtu wa kwanza kufika mwezini afariki dunia

Mtu wa kwanza kutua mwezini afariki dunia
  Neil Armstrong
Mtu wa kwanza kutua mwezini karibu miaka 45 iliyopita Neil Armstrong, amefariki dunia akiwa na miaka 82 weekend hii.
Taarifa za kifo chake zilisambaa kwenye mtandao jana Jumamosi.
Neil Armstrong aliyekuwa injinia amefariki baada ya upasuaji wa moyo siku mbili tu baada ya kutimiza miaka 82.
Rais wa Marekani Barack Obama, ni miongoni mwa watu maarufu waliozungumza baada ya taarifa za kifo chake.
"Neil Armstrong was a hero not just of his time, but of all time. Thank you, Neil, for showing us the power of one small step. -bo," alitweet jana.
Armstrong alikiongoza chombo cha Apollo 11 kilichotua mwezini July 20, 1969.
Source: http://www.janbonline.com

No comments: